Tuesday, 30 September 2014

Ebola yatua Marekani

Mgonjwa wa kwanza wa Ebola Marekani
Mgonjwa wa kwanza wa ugonjwa hatari wa virusi vya Ebola amegundulika nchini Marekani, imethibitishwa katika mji wa Dallas, Texas.
Maafisa katika kituo cha afya cha Texas katika hospitali ya Presbyterian wamesema mgonjwa ambaye hakutajwa ametengwa katika hospitali hiyo.
Mgonjwa huyo anasemekana kuwa ni mtu anayeaminika kuambukizwa ugonjwa huo nchini Liberia kabla ya kuonyesha dalili za ugonjwa huo.
Zaidi ya watu 3,000 tayari wamefariki dunia kutokana na ugonjwa wa Ebola huko Afrika Magharibi na idadi ndogo ya wafanyakazi wa Marekani wa mashirika ya misaada wamepata nafuu baada ya kupelekwa kutibiwa Marekani.
Jumatatu, maafisa wa kituo cha afya cha Texas katika hospitali ya Presbyterian ya Dallas wamesema mgonjwa ambaye hakutajwa jina alikuwa akichunguzwa virusi vya Ebola na ametengwa katika hospitali hiyo.BBC
Shirika la Afya Duniani, WHO limesema mpaka sasa zaidi ya watu 3,000 wamekufa kutokana na virusi vya Ebola, wengi wa waliokufa ni kutoka Liberia.
Nchini Nigeria, nchi yenye idadi kubwa ya watu barani Afrika kuna wagonjwa 19 waliothibitika kuugua ugonjwa wa Ebola na watu wanane wamekufa tangu mgonjwa wa kwanza kuthibitishwa nchini humo mwezi Julai..
Kuna mgonjwa mmoja aliyethibitika nchini Senegal, lakini hakuna taarifa za kifo mpaka sasa.
Ebola ni ugonjwa hatari wa virusi kuwahi kuzuka duniani.

MSAFARA WA KINANA WASAFIRI KWA BAISKELI MILIMA YA USAMBARA KWENDA MKINGA,TANGA

 
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwa na viongozi, waandishi wa habari pamoja na wananchi wakiendesha baiskeli kwenda Kata ya Mg'aro katika mteremko wa milima ya Usambara, akitokea Lushoto kwenda Wilaya ya Mkinga,  mkoani Tanga jana kuendelea na ziara ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM pamoja na kusikiliza kero za wananchi na kutafutia ufumbuzi.

Kinana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye wakiongoza msafara katika safu ya milima ya Usambara kwenda Jimbo la Mkinga, Tanga.

Nyuma ya Nape ni Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Majid Mmanga na nyuma ya Kinana ni Mhariri wa Habari wa gazeti la Jambo Leo, Said Mwishehe.PICHA ZOTE NA KAMANDA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG.(P.T)

Ni safari ndefu lakini yenye faraja na matumaini

Mbele ni Kinana na Mwandishi wa Habari Mwandamizi wa gazeti la Uhuru, Seleman Jongo

Kinana mbele na kutoka kushoto ni wanahabari walio kwenye msafara huo, David John wa Majira, Seleman Jongo wa Uhuru na Said Mwishehe wa Jambo leo pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Majid Mmanga.


Nape akiwasili katika Kata ya Mg'aro mpakani mwa Wilaya ya Lushoto na Mkinga. Pia Kata hiyo inapakana na Kenya.

Kinana na Nape wakifuahi baada ya kuwasili salama baada ya kutumia usafiri wa baiskeli

Wanahabari waliosafiri kwa baiskeli wakipumzika baada ya kufika katika Kata ya Mg'aro

Nape akihutubia wananchi katika Kata ya Mg'aro mpakani mwa wilaya za Lushoto na Mkinga

Watoto wakiwa juu ya kisiki cha mti wakiwa na hamu ya kumuona Katibu Mkuu wa CCM, Kinana akihutubia katika Kata ya Mg'aro.

Kinana akihutubia katika Kijiji cha Mg'aro ambapo aliwahakikishia wananchi wa eneo hilo kuwa barabara ya kutoka Lushoto kwenda Mkinga itaboreshwa, halafu na umeme utawekwa katika Kata hiyo.

Kinana akiagana na Mkuu wa Wilaya ya Lushoto baada ya msafara wake kukabidhiwa kwa uongozi wa Wilaya ya Mkinga katika Kata ya Daluni.

Kinana akiangalia ngoma ya utamaduni iliyokuwa ikitumbuiza wakati wa mapokezi katika Kijiji cha Daluni, wilayani Mkinga.

Kinana akishiriki ujenzi wa jengo la Zahanati katika Kijiji cha Daluni, wilayani Mkinga.

Kinana akisalimiana na wananchi baada ya kuwasili katika Kata ya Maramba.
Kinana akishiriki ujenzi wa jengo la Kituo cha Polisi Maramba
Wananchi wakishangilia baada ya msafara wa Kinana kuwasili katika mkutano wa hadhara katika Kata ya Duga, Uwanja wa Maforoni, wakati wa ziara yake wilayani Mkinga.
Wananchi wakishangilia huku mmoja wapo akiwa na bango la kuisifia CCM katika mkutano huo wa hadhara.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akihutubia katika mkutano wa hadhara katika Uwanja wa Maforoni,  Kata ya Duga.
Kinana akizawadiwa mswala uliotolewa na wanakijiji
Kinana akihutubia katika mkutano huo wa hadhara katika Uwanja wa Maforoni, Duga.

WAFANYABIASHARA MKOANI MBEYA WAFANYA MKUTANO WA KUPINGA MFUMO WA MASHINE YA EFD

nyabiashara mkoani Mbeya akitoa maelezo kuhusiana na agenda ya leseni na tozo mabalimbali kwa wafanyabiashara.


Timu ya watu ya  kutetea haki za wafanyabiashara mkoa wa Mbeya.





Katibu wa wafanyabiashara wilayani Kyela ndg. Musa huseni akitioa maelezo kuhusu mkutano wa JWT unaotarajiwa kufanyika hapa mkoani mwezi huu.

Mamia wa fanyabiashara waliojitokeza kwenye mkutano huo ili kupata ufumbuzi kuhusu swala la mashineya EFD.


Mwenyekiti wa wafanyabiashara wa mkoa wa Mbeya ndg. Charles W. Sionga akitoa maelezo ya maelezo kuhusiana na agenda ya TRA wanatakiwa kusitisha zoezi la ufungaji wa maduka hadi hapo ripoti ya kikao cha tarehe 7/9/2014 kilichofanyika mjini Dodoma .

Wednesday, 24 September 2014

UFAHAMU UNDANI WA NABII TB JOSHUA AMBAYE KANISA LAKE LIMEUA WATU WENGI

Kanisa lililoporomoka mjini Lagos wiki jana na kuwaua watu wengi, lilikuwa linamilikiwa na mhubiri anayesifika sana nchini Nigeria, TB Joshua.
Mwandishi wa BBC Tomi Oladipo anatufichulia haiba ya mhubiri huyu ambaye anadai amewaponya watu wakiwemo vipofu
na waathirika wa HIV.
TB Joshua anadai kuwahi kutabiri matukio mengi kuanzia kwa kifo cha aliyekuwa gwiji wa muziki, Michael Jackson, hadi kupotea kwa ndege ya Malaysia ya MH370.
Anajiita mtume na ni mmoja wa wahubiri mashuhuri sana nchini Nigeria ambako makanisa kama lake ni mengi kupindukia.
Alizaliwa mwaka 1963 tarehe 12 Juni katika familia maskini, akidai kwamba alikaa kwenye tumbo la mamake kwa miezi 15.
Baadaye katika maisha yake, anadai kuona kwenye ndoto yake manabii wakimtaka kuhubiri na kufanya miujiza.
Hapo ndipo alipoanzisha kanisa lake analoiita, 'Church of All Nations (SCOAN),' mwanzoni likiwa na waumini 8.
'Maji ya kuponya'
Watu huja kwake kutoka kote duniani wakitaka kuombewa wapone.Hii leo Jushua kama wahubiri wengine nchini Nigeria, ni tajiri wa kupindukia akishabikiwa sana na watu nchini humo.
Wakati ugonjwa wa Ebola uliporipotiwa katika kanda ya Afrika Magharibi, serikali ya jimbo la Lagos, ilimtambua muhubiri huyo kwa kuambia wagonjwa wa Ebola kwenda kwake akawaponye.
Alikubali kuahirisha baadhi ya programu za kanisa lake za kuponya lakini inaarifiwa alituma chupa 4,000 za maji ya ''uponyo' nchini Sierra Leone anayosema kuwa yanatibu magonjwa mengi tu.
TB Joshua anasema maji hayo ambayo yalitolewa kwa wagonjwa yakiwa ndani ya chupa ndogo, ndogo, yanaweza kuwasaidia wagonjwa kupona na kupata baraka.
'Utabiri'
Katika utabiri wake wa kifo cha Michael Jackson, TB Joshua aliwaambia waumini wake: Katika maeneo yake mwenyewe kuwa yeye ni mashuhuri. "Najulikana kila sehemu." 
Anasifika, kwa unabii wake, TB Joshua anadai kutabiri matukio mbali mbali kuanzia kwa kifo cha marehemu Michael Jackson, hadi kupotea kwa ndege ya Malaysia MH370.
''Kwa sababu mwanzo huwa naona kwamba jambo litamtokea mtu fulani mashuhuri, na kitu hicho kitamalizika, ila huwa sijui tu safari hiyo itakuwa lini. ''
Baada ya kifo cha Michael Jackson, mhubiri huyo alidai kuwa alikuwa amezungumzia kifo cha Jackson miezi sita kabla ya kutokea kwa kifo hicho.
Wakosoaji wake wanasema matamshi na utabiri wake ni wa kubahatisha.
Lakini hili halijawakosesha usingizi waumini wa kanisa lake.
TB Joshua ni mmoja wa wahubiri mashuhuri barani Afrika. Mwanasiasa wa Afrika Kusini, Julius Malema, Rais wa Malawi Joyce Banda, na mwanasiasa wa Zimbabwe, Morgan Tsvangirai na aliyekuwa Rais wa Ghana John Atta Mills, ni miongoni mwa watu mashuhuri ambao wamemtembelea.
Hata Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania, Edward Ngoyayi Lowassa, naye alikwenda huko mwaka 2009. 
Baadhi ya waumini wanadai kufaidika pakubwa kutokana na maombi yake, ni wale wanaosema wameweza kufanikiwa kifedha, kupona na hata watu kufufuliwa.
Nabii Joshua pia anajulikana kwa kazi yake kwa jamii ambayo yeye hujitolea.
Wengi nchini Nigeria hata huhofia kumkosoa TB Joshua. (BBC/MAKALA).

(Nyongeza na Daniel Mbega)
Jina lake halisi anaitwa Temitope Balogun Joshua, lakini anafahamika zaidi kama T.B. Joshua. Alizaliwa Juni 12, 1963 uko Arigidi, Nigeria na anafahamika kama miongoni mwa watu 50 mashuhuri na wenye ushawishi wa Afrika.
TB Joshua ni miongoni mwa wahubiri watano matajiri nchini Nigeria, yeye akishika nafasi ya tatu ambapo utajiri wake unakadiriwa kuwa kati ya Dola 10 - 15 milioni (takriban TShs. 16 - 24 bilioni) akiwa anamiliki kituo cha luninga cha Emmanuel TV na kuuza itabu na kaseti nyingi za mahubiri yake kwa njia ya mtandao. Ni rafiki mkubwa wa Rais wa Ghana John Atta Mills.
Mhubiri anayeongoza kwa utajiri nchini humo ni Askofu David Oyedepo wa kanisa la Living Faith World Outreach Ministry, maarufu kama Winners Chapel alilolianzisha mwaka 1981, ambalo linatajwa kuwa ndilo kubwa zaidi barani Afrika kati ya makanisa ya Kipentekoste. 
Hekalu lake la Faith Tabernacle, ambapo huhudumia ibada tatu kila Jumapili, ndilo hekalu kubwa zaidi la ibada barani Afrika likiwa na uwezo wa kuingiza waumini 50,000 kwa wakati mmoja. 
Anamiliki ndege nne za binafsi na ana majumba London na Marekani. Anamiliki kampuni ya uchapaji ya Dominion Publishing House, ambayo uchapisha vitabu yake. Alianzisha na ndiye mmiliki wa Chuo Kikuu cha Covenant, moja ya vyuo maarufu nchini Nigeria, na shule ya Faith Academy. Utajiri wake kwa sasa ni Dola 150 milioni (takriban TShs. 240 bilioni).
Anayemfuatia kwa utajiri ni Chris Oyakhilome wa kanisa la Believers’ Loveworld Ministries, maarufu kama Christ Embassy. Utajiri wake ni kati ya Dola 30 - 50 milioni (takriban TShs. 48 - 80 bilioni). 
Huyu bwana aliwahi kuwa na kesi ya fedha haramu (money laundering) kiasi cha Dola 35 milioni ambapo alituhumiwa kuzoa fedha kutoka kanisani kwake na kuzificha katika benki mbalimbali nje ya nchi. Hata hivyo, baada ya utetezi, aliachiliwa huru. 
Kanisa lake la Christ Embassy lina wanachama 40,000, miongoni mwao wakiwa matajiri wakubwa na wanasiasa. Anamiliki magazeti, majarida, kituo cha luninga, kampuni ya kurekodi, kituo cha teleisheni cha satellite, hoteli na biashara ya majumba. Kituo chake cha Loveworld TV Network ndicho cha kwanza cha Kikristo kutangaza kwa saa 24 katika mataifa mengi ulimwenguni.
Anayeshika nafasi ya nne ni Matthew Ashimolowo wa kanisa la Kingsway International Christian Centre (KICC), ambaye utajiri wake ni kati ya Dola 6 - 10 milioni. 
Mwaka 1992, kanisa la Foursquare Gospel Church la nchini Nigeria, lilimpeleka Ashimolowo akafungue kituo cha satellite jijini London. Lakini Mchungaji Matthew alikuwa na mawazo tofauti kichwani mwaka na badala yake akaamua kuanzisha kanisa lake.
Leo hii kanisa la Kingsway International Christian Center linatajwa kwamba ndilo kanisa kubwa la Kipentekoste nchini Uingereza. Mwaka 2009, kanisa hilo lilipata faida ya karibu Dola 10 milioni na rasilimali zenye thamani ya Dola 40 milioni. 
Mshahara wake ni Dola 200,000, lakini utajiri wake hasa unatokana na biashara zake nyingine, zikiwemo kampuni yake ya habari iitwayo Matthew Ashimolowo media, ambayo inachapisha habari za Kikristo na vipindi vya aina hiyo.
Mchungaji wa tano kwa utajiri nchini Nigeria ni Chris Okotie wa kanisa la Household of God Church, ambaye utajiri wake unakadiriwa kuwa kati ya Dola 3 - 10 milioni. 
Huyu bwana alipata umaarufu katika miaka ya 1980 wakati alipokuwa mwanamuziki wa miondoko ya pop. Akashukiwa na neema, akaijua Biblia na kuanzisha kanisa la Household of God Church, mojawapo ya makanisa maarufu Nigeria likiwa na washirika 5,000 wakiwemo nyota wengi wa filamu kutoka Nollywood, wanamuziki na watu wengine maarufu katika jamii. 
Aliwahi kuwania urais mara tatu lakini akashindwa kupitia kwenye chama chake alichokianzisha cha Fresh Party. Anapenda matanuzi na anamiliki magari ya kifarahi kama Mercedes S600, Hummer na Porsche

LIVERPOOL YABANWA 2-2, YATOKEA KWENYE PENALTI 14-13 ANFIELD



Mario Balotelli akipambana jana Anfield
KLABU ya Liverpool imeifunga Middlesbrough kwa penalti 14-13 katika Raundi ya Tatu ya Kombe la Ligi, maarufu kama Capital One Cup kufuatia sare ya 2-2 ndani ya dakika 120 Uwanja wa Anfield.
Kinda Jordan Rossiter alianza kuwafungia Wekundu hao baada ya kupewa nafasi ya kwanza kuchezea kikosi cha kwanza, kabla ya Adam Reach kuwasawazishia wageni akimalizia pasi ya Grant Leadbitter.
Mchezo huo ulihamia kwenye muda wa nyongeza kufuatia timu kumaliza zikiwa zimefungana 1-1 baada ya dakika 90.(P.T)

Friday, 19 September 2014

MWANDISHI WA HABARI ITV/RADIO ONE AZIMIA KWA KIPIGO CHA POLISI


Mwandishi wa habari Badi akilia baada ya kushambuliwa na Polisi,huyu ni moja ya waandishi walioshambuliwa

Kuna taarifa kuwa mwaandishi wa habari wa IPP Media kapigwa na jeshi la polisi alipokuwa ameenda kuripoti matukio yaliyokuwa yanaendelea baada ya mwenyekiti wa CHADEMA Mhe, Mbowe alipoenda kuitikia wito wa jeshi hilo la polisi.
Habari zinasema kuwa baada ya Mbowe na wanasheria kuingia ndani polisi walianza kupiga kila aliyekuwa eneo la tukio bila kujali ni nani ndipo alipojikuta mwandishi huyo akipigwa mpaka kupoteza fahamu...(MC)
Imeelezwa kuwa waandishi wengi wa habari wameumia vibaya kutokana na kukimbizwa na mbwa wa polisi huku wengine wakiumwa na mbwa hao.
Waandishi wa habari wameshindwa kutimiza wajibu wao kwa kuzuiwa na polisi ambao wameshindwa kutambua uwepo wa waandishi wa habari,Je Uhuru wa vyombo vya habari uko wapi Tanzania? na kama waandishi wa habari wameanza kuumizwa mapemaa kabisa kabla hata kampeni za uchaguzi hazijaanza,Sijui uchaguzi ukifika hali itakuwaje!!
Ikumbukwe kuwa Mwaka jana mwandishi wa habari Daud Mwangosi aliuawa kikatili kwa amri ya RPC (Kamuhanda) wa Iringa wa wakati huo ambaye baada ya kutimiza azima yake hiyo alipandishwa cheo.
Mami ya watu leo wamejitokeza kumsindikiza Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, baada ya kuhitajiwa kufika Makao Makuu ya Jeshi la Polisi nchini, jijini Dar es Salaam kuhusiana na kauli yake aliyotoa Septemba 14 mwaka huu,juu ya kuitisha maandamano nchi nzima kupinga kuendelea kwa Bunge Maalum la Katiba.
Kilichofuata ni polisi kuamuru watu wote waondoke eneo hilo kwa umbali wa mita 200 ambapo walikimbizwa na mbwa wa polisi na kusababisha wengi wao waumie na kupoteza vitu vyao mbalimbali, hususani wanahabari ambao baadhi yao waliumia na kupoteza zana zao za kazi.
CHANZO; GPL

Tuesday, 16 September 2014

BUNGE MAALUM LA KATIBA YAHITIMISHWA RASMI




Na Benedict Liwenga, MAELEZO-Dodoma
HOJA ya kusitisha Bunge Maalum la Katiba imehitimishwa rasmi Kisheria kwa Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutamka kwamba bunge hilo linaweza kuendelea na shughuli zake.
Taarifa hiyo imetolewa jana 15 Septemba, 2014 na Mjumbe wa Kamati namba Tano, Mhe. Dkt. Asha-Rose-Migiro wakati wa mjadala wa jioni bungeni hapo.
Akisoma taarifa hiyo, Dkt. Migiro amesema kuwa mjadala wa kusitisha bunge umefungwa rasmi hapo jana licha ya kuwepo kwa madai kuwa bunge hilo halina uhalali wa kisiasa.
"Kwaajili ya kuondoa shaka yoyote ningependa kuwaambieni takwimu tulizonazo hivi sasa, bunge hili lina jumla ya Wajumbe 630, kati ya hao waliotoka ni wajumbe 130 ambao ni sawa na asilimia 21% tu ya wajumbe wote, wajumbe waliobaki ndani ya bunge ni 500 hii ni sawa na asilimia 79% ya wajumbe wote na tukizichambua takwimu hizi, ningeomba kutambua wingi wa Kundi la 201", alisema Dkt. Migiro.
Akikanusha juu ya kuwepo kwa dhana iliyojitokeza ya kwamba wajumbe waliobaki ndani ya bunge hilo ni wa aina moja, Dkt. Migiro alisema kuwa taarifa hizo si za kweli, kwani kati ya wajumbe 500 walioko ndani ya bunge hilo wajumbe wanaotokana na kundi la 201 ni wajumbe 189 ambapo wajumbe wanaotoka Tanzania bara jumla yao ni 348 na kati ya hao, 125 ni wajumbe wanaotoka katika kundi hilo la 201.
"Ukitazama takwimu hizi kwa jicho lolote lile basi wajumbe wa 201 ni sehemu kubwa na ni sehemu muhimu ya wajumbe hawa waliobaki", alisema Dkt. Migiro.(Martha Magessa)

BUNGE MAALUM LA KATIBA YAHITIMISHWA RASMI




Na Benedict Liwenga, MAELEZO-Dodoma
HOJA ya kusitisha Bunge Maalum la Katiba imehitimishwa rasmi Kisheria kwa Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutamka kwamba bunge hilo linaweza kuendelea na shughuli zake.
Taarifa hiyo imetolewa jana 15 Septemba, 2014 na Mjumbe wa Kamati namba Tano, Mhe. Dkt. Asha-Rose-Migiro wakati wa mjadala wa jioni bungeni hapo.
Akisoma taarifa hiyo, Dkt. Migiro amesema kuwa mjadala wa kusitisha bunge umefungwa rasmi hapo jana licha ya kuwepo kwa madai kuwa bunge hilo halina uhalali wa kisiasa.
"Kwaajili ya kuondoa shaka yoyote ningependa kuwaambieni takwimu tulizonazo hivi sasa, bunge hili lina jumla ya Wajumbe 630, kati ya hao waliotoka ni wajumbe 130 ambao ni sawa na asilimia 21% tu ya wajumbe wote, wajumbe waliobaki ndani ya bunge ni 500 hii ni sawa na asilimia 79% ya wajumbe wote na tukizichambua takwimu hizi, ningeomba kutambua wingi wa Kundi la 201", alisema Dkt. Migiro.
Akikanusha juu ya kuwepo kwa dhana iliyojitokeza ya kwamba wajumbe waliobaki ndani ya bunge hilo ni wa aina moja, Dkt. Migiro alisema kuwa taarifa hizo si za kweli, kwani kati ya wajumbe 500 walioko ndani ya bunge hilo wajumbe wanaotokana na kundi la 201 ni wajumbe 189 ambapo wajumbe wanaotoka Tanzania bara jumla yao ni 348 na kati ya hao, 125 ni wajumbe wanaotoka katika kundi hilo la 201.
"Ukitazama takwimu hizi kwa jicho lolote lile basi wajumbe wa 201 ni sehemu kubwa na ni sehemu muhimu ya wajumbe hawa waliobaki", alisema Dkt. Migiro.(Martha Magessa)

BUNGE MAALUM LA KATIBA YAHITIMISHWA RASMI




Na Benedict Liwenga, MAELEZO-Dodoma
HOJA ya kusitisha Bunge Maalum la Katiba imehitimishwa rasmi Kisheria kwa Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutamka kwamba bunge hilo linaweza kuendelea na shughuli zake.
Taarifa hiyo imetolewa jana 15 Septemba, 2014 na Mjumbe wa Kamati namba Tano, Mhe. Dkt. Asha-Rose-Migiro wakati wa mjadala wa jioni bungeni hapo.
Akisoma taarifa hiyo, Dkt. Migiro amesema kuwa mjadala wa kusitisha bunge umefungwa rasmi hapo jana licha ya kuwepo kwa madai kuwa bunge hilo halina uhalali wa kisiasa.
"Kwaajili ya kuondoa shaka yoyote ningependa kuwaambieni takwimu tulizonazo hivi sasa, bunge hili lina jumla ya Wajumbe 630, kati ya hao waliotoka ni wajumbe 130 ambao ni sawa na asilimia 21% tu ya wajumbe wote, wajumbe waliobaki ndani ya bunge ni 500 hii ni sawa na asilimia 79% ya wajumbe wote na tukizichambua takwimu hizi, ningeomba kutambua wingi wa Kundi la 201", alisema Dkt. Migiro.
Akikanusha juu ya kuwepo kwa dhana iliyojitokeza ya kwamba wajumbe waliobaki ndani ya bunge hilo ni wa aina moja, Dkt. Migiro alisema kuwa taarifa hizo si za kweli, kwani kati ya wajumbe 500 walioko ndani ya bunge hilo wajumbe wanaotokana na kundi la 201 ni wajumbe 189 ambapo wajumbe wanaotoka Tanzania bara jumla yao ni 348 na kati ya hao, 125 ni wajumbe wanaotoka katika kundi hilo la 201.
"Ukitazama takwimu hizi kwa jicho lolote lile basi wajumbe wa 201 ni sehemu kubwa na ni sehemu muhimu ya wajumbe hawa waliobaki", alisema Dkt. Migiro.(Martha Magessa)

Wednesday, 10 September 2014

NYANGUMI AIBUKA PWANI YA MTWARA, TAZAMA PICHA HIZI HAPA UONE KILICHOTOKEA


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEheAYvttAzgZRGYHn9zcRLkg6JveZ6K-t2WS41KscmKUjDVDhJKzmmrsJjwuemCmjNsc3myD0eapwHrCoZYrAuExNQGgQOXHu_rS8S5a2MrIGGubz8_wlzj3rfpgSeCoZzOsBMi3ucVE-1x/s1600/39036934eea4ff666af2a65b333b9e7b.jpg

Mzoga wa samaki aina ya nyangumi umeibuka katika pwani ya Mtwara leo baada yakukutwa ukielea bahari kuu na wavuvi. Mzoga huo ulivutwa hadi pwani kwa mshangao wa wananchi. Taarifa kamili ya tukio hilo zinatafutwa kwa sasa angalia taswira za mzoga huo

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgSCnM5wUtjPYW_7UICb4TX_ZVpXIjdrkAMk2bYkoMZt1LqxUOHZSfvwxQs-dT3Lc2_VI2eoDzrHZIY3Au7ZMSlwEFdJs7TbTiyQMLeZPevOyiyLqZNNInA6zc0SyFGDG5K0Uxi9mDpzbvL/s1600/861d1cf6d73e46742201ed3cb36d6ce8+(1).jpghttps://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhUptI-Mee3tD55_YmP7GOGlRV7vihYE6KaWhymwZY3eQw3xHiWgMFcaHPeEsISmNAbahGlYvN2_a1KcBP5u4MyIMq4VSRt14YHvlE9YKdV56C2lyElPiBuu6KR07EvDe3j_mBbIiTWzo7L/s1600/f6725c0e2bb75dead8ad32ae0caa1905+(1).jpg

Tuesday, 9 September 2014

Ukatili wa Kutisha: Familia Yateketezwa kwa Moto.....Watoto watatu wafa, mmoja hoi hospitali....



WATOTO watatu wa familia moja, wakazi wa Nyankumbu, Wilaya ya Geita, mkoani Geita, wamefariki dunia usiku wa kuamkia jana baada ya nyumba yao kuteketezwa kwa moto uliowashwa kwa mafuta ya petroli na mtu asiyefahamika.
 
Dada mkubwa wa marehemu hao ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha pili Sekondari Mwatulole na wazazi wao, walijeruhiwa vibaya katika tukio hilo ambalo chanzo chake ni ugomvi wa ardhi.
 
Akizungumza na waandishi wa habari, Mganga Mfawidhi Hospitali ya Wilaya hiyo, Dkt. Adam Sijaona, alisema miili ya watoto hao imehifadhiwa hospitalini hapo.
 
Aliwataja marehemu hao kuwa ni Reginald Robert (9), mwanafunzi wa darasa la nne Shule ya Msingi Nyankumbu Mkombozi, Sophia Robert (6) aliyekuwa akisoma darasa la kwanza shuleni hapo na Remijius Robert (4).
 
Majeruhi ni Scholastica Robert (15), ambaye amejeruhiwa vibaya sehemu mbalimbali za mwili wake ambapo hivi sasa anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando.
 
Wazazi wa watoto hao ambao pia walijeruhiwa katika tukio hilo ni Bi. Angelina Gaspa (36), ambaye amelazwa hospitalini hapo akiwa na majeraha katika mkono wake wa kulia, mgongoni, begani pamoja na Bw.Robert Remijius (45) aliyejeruhiwa kichwani.
 
Akizungumza kwa tabu akiwa wodini, Bi. Gaspa alisema siku ya tukio walikuwa wamelala watoto wakiwa chumbani kwao ambapo ghafla alisikia watoto wakipiga kelele na kusema 'mama tunakufa' na alipokwenda kuwaangalia, akakuta nyumba inateketea kwa moto.
 
"Nilikuta nyumba nzima ikiwaka moto, tulipiga kelele za kuomba msaada kutoka kwa majirani ambao walifika na kuanza kuvunja milango pamoja na ukuta ili waweze kutuokoa.
 
"Mimi na mume wangu tulijitahidi kuvunja tofali japo tupate sehemu ya kupita na majirani walipofanikiwa kuvunja nyumba, tayari watoto wangu watatu walikuwa wameteketea kwa moto,"alisema.
 
Aliongeza kuwa, anaamini chanzo cha tukio hilo ni ugomvi wa ardhi uliokuwepo kati yao na mkazi mmoja wa eneo hilo (jina limehifadhiwa) ambaye alifika na kuchimba kisima katika eneo ambalo wao walilinunua kisheria lakini alidai ni lake.
 
"Tunaishi vizuri na majirani zetu, yote tunamuachia Mungu kwani hata tulipotaka kumlipa ili aondoke katika eneo letu alikataa na mgogoro huu umedumu kwa mwaka mmoja," alisema.
 
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya hiyo, Bw. Manzie Mangochie, alisema kitendo hicho cha kikatili hakitavumilika na aliyefanya tukio hilo lazima asakwe kwa nguvu zote ili aweze kufikishwa katika vyombo vya sheria mara moja.
 
Ofisa Mtendaji wa Kata ya Kalangalala, Bw. Hamad Hussein, alisema watu waliofanya ukatili huo walitumia mafuta ya petroli kuyamwaga mlangoni mwa nyumba hiyo na kusambaa vyumbani ukianzi katika chumba walicholala watoto hao.
 
"Katika eneo la tukio, tumekuta ndoo ya plastiki yenye ujazo wa lita tano iliyotumika kuhifadhia mafuta hayo, tunaomba ushirikiano kwa wananchi ili tuwatie mbaroni wote waliohusika,"alisema.

Mungu saidia Tanzania yetu

10410717_970181069674399_925183454458954453_n

RAIS JAKAYA KIKWETE AKAGUA VIFAA NA ENEO MAALUMU KWA WAGONJWA WA EBOLA JIJINI DAR ES SALAAM




  Baadhi ya wahudumu waliovalia mavazi maalumu wa  wodi maalumu iliyotengwa kwa ajili ya wagonjwa wa ebola iliyoko katika eneo la hospitali ya Temeke  jijini Dar es salaam leo Septemba 9, 2014 mara alipowasili kutokea Dodoma.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwaangalia wahudumu waliopata mafunzo maalumu ya kumhudumia mgonjwa wa ebola wakati alipokagua wodi maalumu iliyotengwa kwa ajili ya wagonjwa wa ebola iliyoko katika eneo la hospitali ya Temeke  jijini Dar es salaam leo Septemba 9, 2014 mara alipowasili kutokea Dodoma.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na wauguzi waliovalia mavazi maalumu tayari kutoa huduma kwa  abiria  atayekutwa na ugonjwa wa ebola  mara atapowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Septemba 9, 2014 mara alipowasili kutokea Dodoma.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo ya jinsi madakrai na wauguzi walivyo jiandaa kufanya ukaguzi wa abiria na kutambua wagonjwa wa ebola mara watapowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jueb4: lius Nyerere jijini Dar es salaam leo Septemba 9, 2014 mara alipowasili kutokea Dodoma.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo ya jinsi vifaa maalumu vinavyofanya kazi ya kutambua wagonjwa wa ebola mara watapowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Septemba 9, 2014 mara alipowasili kutokea Dodoma.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo wakati alipokagua wodi maalumu iliyotengwa kwa ajili ya wagonjwa wa ebola iliyoko katika eneo la hospitali ya Temeke  jijini Dar es salaam leo Septemba 9, 2014 mara alipowasili kutokea Dodoma.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitoa maelekezo ya namna ya kuhudumia abiria wakati wa ukaguzi wa wagonjwa wa ebola mara watapowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Septemba 9, 2014 mara alipowasili kutokea Dodoma.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimsikiliza Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Self Rashid
 Rashid Hemed jinsi Tanzania ilivyojipanga kupambana na ugonjwa hatari wa ebola baada ya kukagua wodi maalumu iliyotengwa kwa ajili ya wagonjwa wa ebola iliyoko katika eneo la hospitali ya Temeke  jijini Dar es salaam leo Septemba 9, 2014 mara alipowasili kutokea Dodoma.Picha na IKULU