Eneo moto ulikotokea |
Wananchi wakishuhudiatukio hilo la moto |
Asikari zima moto wakijitahidi kuzima moto huo. |
eneo lililo nusurika kuungua |
Wananchi wa manispaa ya Iringa kata ya Makorongoni wamekumbwa
na taharuki baada ya moshi mzito kutanda
angani baada ya watu wasiojulikana kuchoma matairi yaliyokuwa yamerundikwa
kwenye jalala hilo lisilo rasmi.
Akizungumza na Habaritalk blog diwani wa kata ya hiyo
Bw.Tadeus Tesha amesema eneo hilo hutumiwa na wachongaji wa viatu vijulikanavyo
kama Kobasi kutupa mabaki
ya matairi ambapo inasemekana kuna watoto wa mtaani hulala kwenye jalala hilo.
Aidha kwa upande wake fundi wa gereji iliyopo jirani
na tukio hilo Bw.Lazaki Wihaa amekana kuhusika kuwa chanzo cha moto huo na
kusema kuwa wachongaji matairihuenda wakawa chanzo.
Mpaka Habaritalk blog inaondoka katika eneo la tukio
chanzo cha moto huo hakikuweza kujulikana kwani uchunguzi wa kina unaendelea.
By Habaritalk blog
No comments:
Post a Comment