Watu wa tatu wanashikiriwa na Jeshi la polisi mkoani
wa Iringa kwa tuhuma ya kusafirisha madawa ya kulevya aina ya mirungi gunia mbili zenye uzito wa
kilogram 121.
Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi Ramadhani Mungi
amesema watuhumiwa hao waliotambulika kwa majina ya Mohamed Ruambo miaka 27
Adam Komba miaka 33 wakazi wa Dares salam na Ayubu Gwalugano miaka 33 makazi wa
Mbeya wamekamatwa leo saa kumi na moja
na nusu alfajiri katika barabara kuu ya Iringa Mbeya eneo la Igumbilo wakiwa
kwenye gari lenye namba T360 SVR mali ya Mwananchi Communication likitokea
Jijini Daers salam kwenda Mbeya .
Aidha Kamanda Mungi amesema kuwa watuhumiwa wanashikiriwa
na Jeshi la polisi kwa uchunguzi.
No comments:
Post a Comment