Wizara ya
Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nchini Tanzania leo imepokea
taarifa kutoka ubalozi wa Libya hapa nchini ikieleza kuwa aliyekuwa
Kaimu Balozi wa Libya Bw. Ismail Nwairat, amefariki dunia jana kwa
kujipiga risasi.
Taarifa
hiyo ya ubalozi imeeleza kuwa kifo hicho kimetokea majira ya saa saba
mchana ofisini kwa kaimu balozi huyo katika jengo la ubalozi wa Lbya
ambapo imeelezwa kuwa marehemu alijifungia ofisini na kujifyatulia
risasi kifuani upande wa kushoto.
Maafisa
ubalozi walivunja mlango waliposikia mlipuko wa bunduki na kumkuta
Kaimu Balozi Nwairat ameanguka chini na kuamua kumkimkimbiza
hospitali ya AMI Oysterbay ambako alitangazwa kuwa amekwisha fariki,
kifo ambacho kimethbitishwa pia na jeshi la polisi
Maiti
imehamishiwa hospitali ya taifa Muhimbili na kwamba ubalozi unafanya
maandalizi ya kusafirisha mwili wa marehemu Nwairat kwenda nchini
Libya kwa mazishi na kwamba serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania imeuhakikishia Ubalozi wa Libya ushirikiano wake katika
kipindi hiki kigumu.
No comments:
Post a Comment