![]() |
Marehemu John Mwankenja, enzi za uhai wake |
Kushoto ni mfungwa, Hakimu Mwakalinga ambaye ni mshtakiwa wa kwanza kuhukumiwa kunyongwa. |
SAUTI KUTOKA NYIKANI.....SERIKALI INAJAZA MAJI YA BOMBA KWENYE KAPU LENYE MATUNDU
GORDON
KALULUNGA
BUNGE la
bajeti linaendelea mjini Dodoma. Kabla ya kuhitimishwa watu wa nyikani
wameniambia niwaeleze wabunge kuhusu tamaa niliyonayo ya kuwa mwalimu wao.
ieleweke kuwa,
kila penye ufa au malalamiko ya watu, kuna watu wananufaika.
Waziri wa
Fedha Saada Mkuya, amesema uchumi umekua kwa asilimia saba. Hapaswi kubishiwa
Waziri huyu na serikali yake.
Asilimia
saba ni uwiano tu, lakini ni zaidi ya hapo. Kila ambaye yupo kwenye kitengo,
uchumi kwake umekua mara dufu na unaendelea kukua.
Kwanza
ijulikane kuwa suala zima la ukusanyaji wa kodi ni gumu sana na lina gharama
kubwa. Kasoro kodi za watumishi zinazokatwa kwenye mishahara.
Kuna makapu
ya (plastic), yenye vitobo vingi, yanayotumika kuwekea takataka maofisini na
nguo chafu kwa wenye uwezo wao.
Pamoja na Serikali
kujipanga na kuendelea kukusanya kodi licha ya kuwepo misamaha mingi kwa
wafanyabiashara wakubwa huku akina mama wauza mboga za majani wakitozwa kodi
kila siku, tatizo lililopo ni ukusanyaji ambao ni sawa na kufungulia bomba,
matarajio yakiwa ni kujaza maji kwenye kapu lenye matobo mengi.
Watu wengi
kwa sasa wanataka kufanyia TRA au kwenye idara za manunuzi (Procurement) kwa
madai kuwa huko wanatoka haraka.
Hayo ni moja
ya makapu ya serikali yaliyo na matundu mengi kwa waliopewa dhamana, huku
serikali ikikazana kufungulia maji bombani huku ikiwa imekinga makapu hayo.
Ngoja
niachane na jambo hili, maana wahusika wanajua fika kuwa najisumbua, kwasababu
hakuna wa kuwawajibisha kwa vitendo katika nyika yetu.
Kabla ya
kumalizika kikao cha Bunge la bajeti, natamani kuwa Mwalimu katika shule
iitwayo Bunge na wanafunzi waitwao waBungwe. Kabla ya kumaliza vikao ningempa
kila mmoja kazi yake ya kufanya nyumbani (jimboni).
Baadhi nina
uhakika kuwa wangefaulu vizuri ingawa sisemi kuwa wengine wangefeli. Singida
mjini Mohamed Dewji, Zungu, Monduli
Edward Lowassa na wewe, sijui kwanini nimewataja viongozi hawa kwa majina,
lakini tuliache kama lilivyojitokeza.
Ingenichukua
muda kusahihisha kazi hizo za nyumbani (Homeworks), lakini wote wangefanya vema,
Tanzania yangu ingekuwa sehemu bora ya kuishi kuliko ilivyo sasa.
Napenda mfumo
wa ufundishaji wa walimu wa zamani "old style" ya ualimu. Ile
waliyokuwa wakiifanya waalimu kama Baba yangu Mwalimu mstaafu, Frank Burton Kalulunga,
ambapo walimu walikuwa wanajua uwezo wa kila mwanafunzi.
Walikuwa
wanahakikisha kuwa kila mwanafunzi anafanya kazi aliyopewa na walikuwa
wanasahihisha siku inayofuata.
Walikuwa na
uwezo wa kutambua kama mwanafunzi kafanya mwenyewe ama amefanyiwa. Baada ya
kusahisha, walikuwa wakibandika matokeo.
Shabaha
ilikuwa ni kujua nani kawa wa kwanza na nani wa mwisho. Hapo ilikuwa ni lazima mwanafunzi
asome sana ili aweze kupata Vema.
Mfumo ule
ulikuwa na faida, maana yaliyotendeka ilikuwa ni changamoto kwa kila mwanafunzi
kuongeza juhudi katika masomo.
Mfumo huu
ningeupata na kuweza kuutumia katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
naamini ingesaidia sana.
Ningehakikisha
kila Mbunge anapoondoka bungeni baada ya kusanyiko anapewa kazi ya kufanya
jimboni mwake na akirejea "darasani" (kikao) kijacho, kwanza
ninaangalia nani kafanya nini na kafanikiwa mangapi kisha tunasonga mbele.
Lengo ni kujua
nani anajua na kutatua matatizo ya jimboni mwake na kuwasaidia wapiga kura wake
na pia tungejua nani hana ajualo kuhusu shida na mahitaji halisi ya waliomchagua.
Ingetuwezesha
kujua nani yuko mstari wa mbele kubadilishana mawazo pale nitakapowapa kazi za
makundi, kukokotoa maswali na kutumia maarifa ya wenzake kufanya kazi zake
kuwasaidia wapiga kura wake.
Nina uhakika
kwa mfumo huu lazima nchi yangu ingeinuka na kuanza kusimama dede na kutupa
mguu mbele kuelekea kwenye mafanikio ya mahitaji halisi ya wapiga kura.
Licha ya
kuwapa hizo kazi za nyumbani, ningewapa wabunge (wanafunzi) wangu, jukumu la
kusaka mahitaji ya wahitaji ambao kwa bahati mbaya baadhi wameonekana kujisahau
kuyaweka bayana.
Nigejaribu
kuwashawishi "maafisa elimu" kuhakikisha mchujo wa kujiunga na shule
(uchaguzi) unafanyika kwa nyakati tofauti kwa faida na sababu nilizozieleza.
Ningewapa
mtihani wa kila Mbunge kuwa na kiwango cha chini cha kuishi jimboni mwake kila
mwaka, kwasababu wapo wabunge ambao wanaenda majimboni kwa nadra sana.
Mtihani
mwingine ungekuwa ni kushinikiza wabunge kufanya mikutano sehemu zote ambazo
waliomba kura kabla na baada ya kuhudhuria vikao vya bunge.
Wengi
wanapokutana bungeni wanasema mahitaji ya jimbo sijajua kwa mujibu wa
nani,(sisemi kwa mujibu wa wananchi na wala sisemi kwa mujibu wa wao).
Sina imani
kwa sasa kama wabunge wanapoondoka bungeni kama wanapewa majukumu ya
kutekeleza, ama wakipewa wanaweza kuyatekeleza bila kuwaeleza wananchi? Lakini
kama ni majukumu kwa wananchi si tungeona mabadiliko huko tuliko?
Namaanisha
hata kama hatuambiwi si tungejua kuwa "ujenzi wa hizi zahanati ni manufaa
ya m'bunge kwenda kwenye kikao / vikao vya mwaka huu?
Kuna
mwananchi anayeweza kujibu akiulizwa amenufaika nini na m'bunge wake kwenda
kwenye vikao vya kila mwaka? Sisemi hatujanufaika, (japokuwa sisemi kuwa tumenufaika),
sijui tufikirieje matumizi ya kodi zetu?
Kama
mwalimu, ningehakikisha maswali yanajibiwa na kazi zangu zote zingefanyika na
naamini mwisho wa muhula ningebandika matokeo, pia kuyatuma kwa wazazi
(wananchi) ili wajue maendeleo ya wanafunzi na kujua nini cha kuwafanya katika
muhula ujao wa shule (mhula wa uchaguzi).
No comments:
Post a Comment