Mkali
wa muziki wa rege nchini, Innocent Nyanyagwa na bendi yake wakitumbuiza
kwenye tamasha la 17 la ZIFF 2014 linaloendelea kwenye viunga vya Ngome
Kongwe visiwani Zanzibar.(Picha zote na Zainul Mzige wa MOblog).
Na. Mwandishi wetu, Zanzibar
MKALI wa
muziki wa rege nchini Innocent Nganyagwa anajiandaa kutoa filamu
inayohusu maisha yake kama sehemu ya kufunza kizazi kijacho kuhusu
muziki huo.
Filamu hiyo ambayo itabeba maisha yake ya kuishi katika muziki wa rege inatolewa kama ile ya Jimmy Clief The hader they Come.
Nganyagwa
mwenye albamu nne na tuzo tano za hapa nyumbani alisema pamoja na kukaa
kimya kwa muda mrefu alikuwa hajaondoka katika muziki wa rege lakini
alikuwa anafundisha vijana ili rege iwe na undelevu nchini.
Nganyagwa
ambaye alitumbuiza kwenye viunga vya Mambo Club iliyopo Ngome Kongwe
amesema kwamba amekuja katika tamasha la ZIFF akiwa na mpya nyingi
kuonesha wazi kwamba hakuwa mkaa bure.
Akijibu
swali kuhusu mahadhi ya muziki wake na imani yake ya kirastafarian
amesema kwamba muziki wa rege japo upo ndani ya imani ya kirasta,
unasimama wenyewe ndio maana mtu kama yeye hapigi rege ya Jamaica kama
ilivyokuwa kwa Jimmy Clief, Burning Spear au Bob Marley.
Amesema
muziki wake ni wa kitanzania kwa sababu taifa hili lina vionjo vingi vya
kufanya katika kuuza utamaduni wake nje kupitia muziki.
Amesema
japo miondoko ya mfumo wa Babylon bado ipo kuna mstari mwembamba sana
kati ya dini ya rasta na muziki wa rege na mwitikio wa muziki wa
ukombozi.Hata hivyo amesema kwamba sasa hivi anapiga muziki ‘mtamu’
(sweetie reggae) muziki wa mapenzi.
Innocent
Nyanyagwa na Back Vocalist wake wakishambulia kwenye tamasha la 17 la
ZIFF 2014 ndani ukumbi wa Mambo Club-Ngome Kongwe.
Akizungumza
uuzaji wa muziki wa Tanzania nje, amesema ipo haja ya wasanii kuacha
kukopi na kupest (kunakiri) kwani kwa kufanya hivyo hawauzi utamaduni na
hivyo wanainyima nchi fursa ya kujulikana mwisho.
“Ipo haja ya kutangaza utamaduni wetu” alisema Nganyagwa.
Aidha
aliitaka serikali kuwekeza katika muziki kwa kuingilia usambazaji wa
bidhaa hizo ili wasanii waweze kunufaika zaidi kuliko sasa.
Ras Inno
akiwapa mzuka mashabiki wake kwa kuruka na wamasai ndani ya Ngome Kongwe
alipotoa show ya aina yake baada ya kuhudhuria tamasha la ZIFF miaka
nane iliyopita.
Watu weweeee....Haire rastafarai.....full mzuka babaake.!
No comments:
Post a Comment