Kamanda wa Polisi, Kikosi cha Usalama Barabarani DCP Mohammed Mpinga
WAKATI
Rais Jakaya Kikwete akiungana na Watanzania kuomboleza vifo vya watu 19
walioteketea katika ajali ya basi lililoungua moto baada ya kugongana na
lori juzi mjini Morogoro, imefahamika kuwa, ajali za barabarani
zimegharimu maisha ya watu 969 kati ya Januari Mosi na Aprili 12 mwaka
huu.
Aidha,
watu 2,500 wamejeruhiwa katika kipindi hicho, wengine wakisababishiwa
ulemavu wa kudumu kutokana na ajali hizo. Hii ina maana kwamba, kwa
wastani, watu 10 walipoteza maisha katika ajali za barabarani kila siku
kati ya Januari na Aprili 12 mwaka huu, ilhali waliojeruhiwa ni wastani
wa watu 25 katika muda kama huo.
Hayo
yalibainishwa jana na Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Nchini,
Mohammed Mpinga aliyesema hayo yametokea katika ajali za barabarani
2,224 za kati ya Januari na mwanzoni mwa Aprili.
Alisema
watu 866 walikufa na wengine 2,363 kujeruhiwa kati ya Januari na Machi,
wakati wengine 103 wamepoteza maisha na 138 kujeruhiwa kati ya Machi 11
na Aprili 12 mwaka huu.
Alisema
katika ajali zote hizi chanzo kikubwa ni mwendokasi wa madereva bila
kuzingatia alama na michoro ya barabarani na abiria kushabikia mwendo
kasi na kumtetea dereva pindi anapofanya makosa.
"Dereva
akifanya makosa akikamatwa abiria wanachangia kumlipia faini dereva
jambo ambalo linawapa madereva kiburi wakiamini akifanya makosa abiria
wanamsaidia," alisema Mpinga.
Aliongeza
kuwa kwa upande mwingine wamiliki wa vyombo vya usafiri wanachangia
ajali kwani wamekuwa wakiwadhibiti na kuwaamrisha madereva wao kwenda
mwendo kasi na pale anapokosea anamlipia faini jambo ambalo linapelekea
kutokea kwa ajali zinazopoteza maisha ya watu wengi na kuwaachia wengine
vilema vya maisha.
No comments:
Post a Comment