Tuesday, 3 February 2015

HATIMAYE OMEGA MEDIA PRODUCTION YATUA ARUSHA NA BAHATI BUKUKU

Kilio cha wengi jijini Arusha hatimaye kimepata mfuta machozi ni Omega Media Production ni baada ya kufanya matamasha mengi mikoani sasa ni zamu ya Arusha katika kuiweka wakfu albam ya mtoto Miriam Paul mwenye umri wa miaka  8 akiwa na uwezo wa ajabu wa kumwimbia Mungu na kulitawala jukwaa kwa kutumia talanta alizopewa na Mungu wa mbinguni.

Tamasha hili litafanyika jumapili ya tarehe 8/02/2015 katika kanisa la katoliki kijenge Arusha mjini kuanzia saa 8 mchana na kuendelea wakati huo huo atasindikizwa na waimbaji mbalimbali kama Bahati Bukuku Tumsifu Rufutu (mzee wa mwambie farao),Fred Ndumbaro,Redemption Tarimo,Mary Masonga,Beatrice Mwakalinga, Joseph Roma na Rose Paul bila kusahau  ENG.Carlos Mkundi na wengineo wengi.

No comments:

Post a Comment