Tuesday, 3 February 2015

BONDIA FRANCIS CHEKA AHUKUMIWA JELA MIAKA 3


 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgb6tN_Yztflt9xmznGAMENYMD4mRW9na4TaIRD0TcGaKaAYP1p9ernAA2azXfnZpmfu-LetT8joGS-WPlctoiDlo67_nLHiNk3Giug23s-439QB-5iw4kLnVH-BbW7MVSfkICiTm3xhag/s640/Bondia-Francis-Cheka.jpg
Bondia Francis Cheka leo February 2 2015 amehukumiwa kwenda jela miaka mitatu na faini ya Milioni moja laki sita kwa kosa la kumpiga mmoja kati ya wafanyakazi wake
kwenye bar yake iliyopo Morogoro.

cheka

Muda mfupi uliopita Francis Cheka ameongea na millardayo.com na kusema ndio alikua anajiandaa kuachia simu yake na vitu vingine muhimu ili achukue karandinga kuelekea gerezani ambapo namnukuu akisema ‘imeshakua hivi tayari ila hamna noma, niko na wanangu wengine wamepigwa miaka 10 nitakua nao fresh tu ila hamna noma ni miaka mitatu tu mimi’

Hukumu imetolewa na Hakimu Mkazi Said Msuya ambapo baada ya hayo upande wa Francis Cheka unasemekana kujiandaa kukata rufaa.

Unaweza kubonyeza play hapa chini kumsikiliza Ahmad Machaku akiripoti kutoka Morogoro.

HATIMAYE OMEGA MEDIA PRODUCTION YATUA ARUSHA NA BAHATI BUKUKU

Kilio cha wengi jijini Arusha hatimaye kimepata mfuta machozi ni Omega Media Production ni baada ya kufanya matamasha mengi mikoani sasa ni zamu ya Arusha katika kuiweka wakfu albam ya mtoto Miriam Paul mwenye umri wa miaka  8 akiwa na uwezo wa ajabu wa kumwimbia Mungu na kulitawala jukwaa kwa kutumia talanta alizopewa na Mungu wa mbinguni.

Tamasha hili litafanyika jumapili ya tarehe 8/02/2015 katika kanisa la katoliki kijenge Arusha mjini kuanzia saa 8 mchana na kuendelea wakati huo huo atasindikizwa na waimbaji mbalimbali kama Bahati Bukuku Tumsifu Rufutu (mzee wa mwambie farao),Fred Ndumbaro,Redemption Tarimo,Mary Masonga,Beatrice Mwakalinga, Joseph Roma na Rose Paul bila kusahau  ENG.Carlos Mkundi na wengineo wengi.