Wednesday, 22 October 2014

Oscar Pistorius ahukumiwa kifungo cha miaka 5 jela


Mahakama ya Afrika Kusini imemhukumu kifungo cha miaka 5 jela mwanariadha mlemavu Oscar Pistorius kwa kosa la kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp.

Mwezi September, mahakama hiyo ilimkuta Pistorius na hatia ya kumuua Reeva Steenkamp bila kukusudia katika siku ya wapendanao mwaka jana (February 14,2013).

Pistorius alikiri kumpiga risasi Reeva nyumbani kwake na kujitetea kuwa alidhani ni mtu aliyevamia nyumbani kwao usiku ule.
Akitoa masharti ya hukumu hiyo, jaji ameeleza kuwa Pistorius anapaswa kutumikia angalau 1/6 (Miezi 10) ya adhabu yake kabla hajafikiriwa kwa lolote.

Monday, 6 October 2014

MJUE IRENE LA VEDA, MSHIRIKI WA BBA KUTOKA TANZANIA



 
Irene Neema Vedastous 'La Veda', Mshiriki wa Big Brother Hotshots kutoka Tanzania.
IRENE NEEMA VEDASTOUS ni msichana mrembo wa Kitanzania, mwenye umri wa miaka 23 anayeiwakilisha Tanzania katika shindano la BIG BROTHER 2014 ‘HOTSHOTS’ nchini Afrika Kusini.
La Veda katika pozi na baadhi ya mastaa.
Mrembo huyu ambaye ameshawahi kuingia 10 bora ya shindano la Miss Tanzania mwaka 2012, baada ya kutwaa taji la Miss Lindi 2012, anaingia rasmi leo tarehe 5 Oktoba 2014 kwenye shindano hilo lenye mashabiki
wengi duniani ambalo kuanzia saa 1 jioni litakua likirushwa live kupitia DSTV kwenye channel no. 198.
Irene Neema Vedastous aka Irene La Veda ni nani?(P.T)