Na Hudugu Ng'amilo
Wabunge
wa Chama Cha Mapinduzi jana waliipinga hadharani bajeti ya Serikali
inayoendelea kujadiliwa bungeni, kwa madai hawatakuwa tayari kuiunga
mkono kwa kuwa haina jipya.
Wabunge
hao ni Anne Kilango (Same Mashariki), Kangi Lugola (Mwibara) na Mbunge
wa Viti Maalumu Vicky Kamata ambao kwa nyakati tofauti walisema kuunga
mkono bajeti hiyo ambayo haitekelezeki ni sawa na kuwasaliti wananchi
wao.
Lugola
alitoa sababu za kutounga mkono bajeti hiyo kwa kuwa ni 'bajeti
mchepuko' yenye vipaumbele lukuki lakini havitekelezi hata kimoja.
Mbunge
huyo alitoa sababu zaidi ya saba za kutounga mkono, akisema ni mwiko kwa
mbunge makini kuunga mkono bajeti kama ilivyo sasa kwa kuwa anatambua
hakuna kitakachofanyika wakati wote wa utekelezaji.
"Nimeipa
jina la bajeti mchepuko kwa sababu nyingi, la muhimu ni kuwa bajeti hii
imejaza vipaumbele vingi ambavyo kwa mtazamo wangu havitatekelezeka hata
siku moja," alisema Lugola.
Niweke
wazi tu hapa kuwa, kama mtalazimisha mambo mengine ikiwamo misamaha ya
kodi, nitakuwa tayari kutumia ubaunsa wangu humu ndani kupambana na
mbunge yeyote anayepinga kufutwa kwa misamaha ya kodi,"alisema Lugola.
"Kama
hamtaleta sheria ili tumpe meno kamishina wa madini, nakwenda Mwibara
kuwahamasisha wavuvi siku mkiwakamata na nyavu au makokoro wagome hadi
uchunguzi ufanyike kwanza."
Kwa
upande wake, Vick Kamata alitoa sababu za kutounga mkono ni kutokana na
kile alichokiita udanganyifu wa Serikali kwa wachimbaji wadogo ambao
wameshindwa kupata msaada wakati wote.
Alisema
Serikali imekuwa ikiwatengea maeneo ambayo hayana dhahabu kabisa na
matokeo yake wanachimba hadi wanazeeka bila ya kupata dhahabu wakati
ikiendelea kuwabeba wakubwa na matajiri.
Naye
Kilango alisema sababu kuu ya kupinga ni hadi pale Serikali
itakapoongeza fedha katika Wizara ya Afya ili iweze kulinda afya za
Watanzania wanyonge wakiwamo akina mama na watoto jimboni kwake.
CHANZO MWANANCHI
CHANZO MWANANCHI
No comments:
Post a Comment