Sunday, 29 June 2014

Van Gaal; Kopo la maji uwanjani ?


 
140623151406_van_gaal_wc2014_512x288_afp_nocredit_b590c.jpg
140618182130_van_persie_gaal_wc2014_512x288_afp_nocredit_74b89.jpg
Van Gaal kiwango cha joto ni juu mno
Kocha wa Uholanzi Louis van Gaal anatarajia shirikisho la soka duniani FIFA litawaruhusu wachezaji wake kunywa maji katika mechi yao ya raundi ya pili dhidi ya Mexico itakayochezwa katika uwanja wa Castelao ulioko katika eneo la Fortaleza.
Fortaleza ni eneo linaloshuhudia viwango vya juu vya nyuzi joto.
Kocha huyo wa Manchester United ya Uingereza anasema kuwa utafiti uliofanywa kabla ya mashindano haya yanasema kuwa wachezaji wanapoteza maji lita nne ama zaidi kwa kila mechi wanayocheza katika jimbo hilo la Fortaleza.
Ni dhahiri kuwa mwili wa binadamu yeyote unastahili maji kwa hivyo hawa wachezaji naamini kuwa wanastahili kunywa maji ilikuzuia wasishikwe na kisunzi .
Van Gaal alitishia kuwapa wachezaji wake maji kwa wingi kando kando mwa uwanja iwapo FIFA haitahalalisha kuwepo kwa dakika moja au mbili ambapo mechi zitasimamishwa iliwachezaji wake wapige kopo la maji.
Kiungo wao Leroy Fer, ambaye anauguza jeraha la goti anasema kuwa Uholanzi ilipata kionjo tu cha kucheza katika hali ya kiwango cha juu mno cha joto baada ya kuwasili huko wakitoka Rio de Janeiro.
Fer anasema kuwa japo Uholanzi imezoea kucheza katika maeneo ya Uropa yenye baridi kali,Uholanzi itajikaza kisabuni kwani ni hali ileile itakayoikumba timu pinzani ya Mexico.(A.I).

No comments:

Post a Comment