Sunday, 29 June 2014

Utoro BLW wakwamisha bajeti Z’bar



670_bd867.png
Baraza la Wawakilishi Zanzibar (BLW) limekwama kukaa kama kamati ya matumizi na vikao kwa mara ya tano tangu kuanza kujadili bajeti za mwaka wa fedha 2014/15 Mei 14 mwaka huu kutokana na tatizo la wajumbe kuwa watoro wa kuhudhuria vikao.
Hali hiyo imekuwa ikimlazimu Spika wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Ameir Kificho, Naibu Spika Ali Abdallah Ali na Mwenyekiti wa Baraza hilo Mgeni Hassan Juma kushindwa kuitisha Kamati ya Matumizi kutokana na kutotimia akidi ya asilimia 50 ya wajumbe 40 kati ya wajumbe 82.
Tukio la aina hiyo lililotokea mwishoni mwa wiki baada ya Naibu Spika Ali Abdallah Ali kujikuta akiahirisha Baraza hilo kutokana na uchache wa wajumbe wakati wakijadili bajeti ya Wizara ya Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati iliyowasilishwa na Waziri Ramadhan Abdallah Shaaban.(P.T)

No comments:

Post a Comment