Monday, 16 June 2014

UGONJWA WA DENGUE WAANZA KUPUNGUA

Serikali ya Tanzania imesema ugonjwa wa dengue umeonekana kuanza
kupungua katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania kutokana na wananchi kuchukua tahadhari kuhusu ugonjwa huo.

Akiongea na mtandao wetu Msemaji wa Wizara ya Afya na Ustawi wa
Jamii, Nsachris Mwamwaja amesema mpaka siku ya jana wagonjwa wawili
pekee waliokuwa wamelazwa na mmoja kuthibitika kuugua ugonjwa huo.
Aidha, Mwamwaja amewataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari kwa kusafisha mazingira ili kutokomeza kabisa ugonjwa huo.

No comments:

Post a Comment