Na Fadhy Mtanga 27 Juni 2014
Wakati
anatakiwa kulipa faini ya paundi 64, 000/= kama sehemu ya adhabu ya
FIFA, makampuni yameanza kuvunja mkataba na nyota huyo wa Uruguay.
Kampuni
ya kamari ya 888 kutoka Gilbraltar imevunja rasmi mahusiano yake ya
kibiashara na nyota huyo. Tayari kampuni ya vifaa vya michezo ya Adidas
imeondoa matangazo yote ya Kombe la Dunia yenye picha za Luis Suarez.
Adidas pia wamesema watapitia upya mahusiano yao ya kibiashara na nyota
huyo mara baada ya kumalizika kwa fainali zinazoendelea nchini Brazil.
Adidas ni washirika wakubwa sana wa FIFA. Katika taarifa yao, wamesema
wanaiunga mkono FIFA.
Kampuni
ya vifaa vya michezo ya Warrior Football inayotengeneza jezi
zinazotumiwa na Liverpool nayo ipo katika mchakato wa ndani wa kufanya
maamuzi juu ya uhusiano wake kibiashara na nyota huyo.
Wadhamini wa fulana za Liverpool, Standard Chartered wanatarajiwa pia kutoa msimamo wao.
Klabu ya
Barcelona inatumia mwanya wa adhabu ya Suarez kumshusha dau hadi paundi
milioni 50 kutoka bei yake kabla ya sakata ya paundi milioni 87.5
Luis
Suarez amepigwa kufuri la kutojihusisha na kandanda kwa miezi minne,
kutocheza mechi 9 za kimataifa baada ya kupatikana na hatia ya kumpiga
meno mlinzi wa Italy mataifa hayo yalipokwaana katika michuano ya Kombe
la Dunia mapema wiki hii.(P.T)
No comments:
Post a Comment